Tanzania imepata bahati ya kufikiwa na Programu ya UEFA ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu (UEFA Assist) ambapo imeandaliwa semina maalum yenye lengo la kuboresha Ligi za Tanzania na Uendeshaji wa Mashindano nchini.
Programu hiyo ilianza Novemba 2021 kwa zoezi la kukusanya maoni ya wadau mbalimbali wakiwemo makocha, wachezaji, Wanahabari, viongozi wa Shirikisho na Bodi ya Ligi, viongozi wa klabu, wadhamini na washabiki.
Hatua ya pili ya Programu hiyo ni semina ambayo itaendeshwa na maafisa wa UEFA Assist kwenye hoteli ya Golden Tulip mkoani Dar es salaam kuanzia Januari 10 hadi 15, 2022.
Washiriki wa semina hiyo ni viongozi na maafisa wa TFF na Bodi ya Ligi, viongozi na maafisa wa klabu za Ligi Kuu (Mwenyekiti/Rais, Katibu/CEO, Mkurugenzi wa Ufundi na Afisa wa Fedha na Mipango).
Baada ya semina hiyo, Programu itaingia katika hatua ya tatu ambapo maafisa wa UEFA Assist watasimamia utekelezaji wa mapendekezo ya maboresho Ligi na Uendeshaji wa Mashindano nchini.