SEMINA ya Maendeleo ya Ligi inayoendeshwa na UEFA chini ya mradi wao wa UEFA Assist imeingia siku ya nne leo kwenye Hotel ya Golden Tulip iliyopo Dar es Salaam.
Leo washiriki wa semina hiyo inayotarajiwa kukamilika Januari 15, 2022, wamepata nafasi ya kujifunza masuala mbalimbali zikiwemo mbinu za kuziongezea kipato klabu zao.

Semina hiyo inashirikisha viongozi na maafisa wa TFF na Bodi ya Ligi, viongozi na maafisa wa Klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya NBC, wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bodi ya Ligi.