Ligi kuu ya NBC inaendelea hii leo kwa michezo miwili ya raundi ya nne, saa 10:00 alasiri Mbeya City watawaalika Azam FC kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Kwenye michezo mitano ya mwisho ya Ligi Kuu kwa timu hizi kukutana, Azam wameshinda mara tatu, Mbeya City wakishinda mchezo mmoja huku wakitoka sare mchezo mmoja.
Saa 1:00 usiku kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, Yanga SC watawakabili Mtibwa Sugar.
Kwenye msimamo wa Ligi ya NBC Mtibwa Sugar wapo nafasi ya pili wakiwa na alama saba sawa na Yanga wenye alama saba, timu yoyote itakayopata ushindi kwenye mchezo wa leo itapanda moja kwa moja kwenye nafasi ya kwanza ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.