SIMBA, PRISONS NI REKODI NA HISTORIA LEO MBEYA,YANGA YAPANDA KILELENI

Kivumbi cha raundi ya nne ya Ligi Kuu ya NBC kinaendelea leo kwa mchezo mmoja kati ya Tanzania Prisons na Simba utakaochezwa saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Mchezo wa mwisho kwa timu hizi kukutana ilikuwa ni Juni 26, 2022 kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya na Tanzania Prisons kuibuka na ushindi wa bao moja lililofungwa na Benjamin Asukile.

Mara ya mwisho kwa Simba kupata matokeo katika uwanja ugenini dhidi ya Tanzania Prisons ilikuwa ni Mei 5, 2019 waliposhinda kwa bao moja.

Jana michezo miwili ya raundi ya nne ilichezwa, Mbeya City wakiwaalika Azam FC ulitamatika kwa Azam kushinda kwa bao moja, Saa 1:00 usiku Yanga SC waliwakabili Mtibwa Sugar na kumalizika kwa Yanga kushinda kwa mabao matatu, ushindi huo unawapandisha Yanga hadi nafasi ya kwanza ya msimamo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *