MTIBWA YAISHUSHA MBEYA CITY, PRISONS HOI

TIMU ya Mtibwa Sugar imefanikiwa kuishusha timu ya Mbeya City katika nafasi nne za juu katika msimamo wa Ligi baada ya kuifunga Polisi Tanzania bao 2-1.

Polisi Tanzania ilikua ya kwanza kuandika bao kupitia kwa Ambrose Awio dakika ya 35 huku mabao ya Mtibwa yakifungwa na Ismail Mhesa dakika 45 kabla ya Onesmo Mayaya kufunga la pili dakika ya 48.

Huu ni mchezo wa pili mfululizo kwa Mtibwa kupata ushindi nyumbani ikiwa ni baada ya kuifunga timu ya Coastal Union idadi hiyo ya mabao katika raundi ya 12.

Ushindi huo unaisogeza Mtibwa nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu NBC kwa kufikisha pointi 21 ikiizidi Mbeya City kwa pointi tatu na mchezo mmoja.

Mkoani Mbeya Tanzania Prisons imeendelea kusuasua baada ya kupoteza mechi dhidi ya Kagera Sugar kwa bao 1-0 lililofungwa na Meshack Mwamita dakika ya 85 kwa shuti la mbali lililomshinda golikipa Edward Mwakyusa.

Timu ya Tanzania Prisons imepoteza mchezo wa tatu mfululizo iliyocheza nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar huku wakishuka mpaka nafasi ya 11 katika msimamo wa Ligi Kuu NBC.

Bada ya ushindi huo Kagera Sugar imepanda hadi nafasi ya tisa kwa kufikisha pointi 15 bila mchezo wowote mkononi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *