PRISONS YAMALIZA UBABE WA GEITA NYANKUMBU

TIMU ya Prisons ya Mbeya imemaliza ubabe wa Geita Gold ikicheza katika uwanja wake wa Nyankumbu kwa kuifunga Mabao 3-1.

Mchezo wa mwisho kwa Geita kufungwa uwanja wa Nyankumbu kabla ya kipigo cha leo ilikua dhidi ya timu ya Pamba kutoka Mwanza katika mchezo wa Ligi ya Championship msimu wa 2020/21.

Mabao ya Jeremiah Juma, Samson Mbangula na Edwin Balua yameifanya Prisons kuwa timu ya kwanza kuondoka na alama zote tatu dhidi ya Geita Gold kwenye uwanja wa Nyankumbu tangu timu hiyo ipande daraja.

Ushindi huo ni wa tatu mfululizo kwa timu ya Prisons ikipanda hadi nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kukusanya alama 31.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *