RHINO YAANZA KIBABE, TMA IKIENDELEZA REKODI

TIMU ya Rhino Rangers ya Tabora imeanza kibabe mashindano ya First League hatua ya Nane Bora kwa kutoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya African Lyon ya Dar kwenye mchezo wa kundi B uliopigwa saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Azam.

Pamoja na African Lyon kutangulia kupata bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Agiri Ngoda walishindwa kuhimili mashambulizi ya Rhino waliosawazisha kupitia kwa Ramadhan Abdallah na kupata bao la ushindi dakika ya mwisho lililofungwa na Masawe Masawe.

TMA Stars ya Arusha ilicheza na Dar City ya Dar es Salaam saa 1:00 usiku ikiwa ni mchezo wa pili wa kundi B uliomalizika kwa suluhu.

TMA imeendeleza rekodi ya kutopoteza mchezo wowote wa First League msimu huu mpaka kufikia hatua ya Nane Bora huku ikiwa timu iliyoruhusu mabao machache (9).

Rhino Rangers baada ya ushindi wa leo wanashika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa kundi B wakifuatiwa na Dar City na TMA wenye alama moja kila timu baada ya sare ya leo huku nafasi ya mwisho ikishikwa na African Lyon.

Ligi hiyo itaendelea tena Aprili 26 kwa michezo miwili ya kundi A itakayokutanisha timu za Lipuli dhidi ya Alliance mchezo wa saa 10:00 alasiri na Cosmopolitan itakua mwenyeji wa Stand United saa 1:00 usiku.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *