LIPULI, ALLIANCE HAKUNA MBABE, STAND YATINGA NUSU FAINALI

TIMU ya Lipuli ya Iringa ililazimika kusubiri hadi dakika ya 90 kupata bao la kusawazisha dhidi ya Alliance ya Mwanza na kufanikiwa kutoka na sare ya bao 1-1 katika mchezo wa First League hatua ya Nane Bora.

Alliance ilikua ya kwanza kupata bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Benjamin Williams dakika ya 32 kabla ya Hemed Ally kuifungia Lipuli kwa mpira wa adhabu uliomshinda golikipa wa Alliance.

Matokeo hayo yanaweka hai matumaini ya timu hizo mbili kusonga mbele hatua ya nusu fainali ikiwa timu mojawapo itashinda mchezo wa mwisho na kuongoza kwa idadi kubwa ya mabao ya kufunga.

Stand United ya Tabora imefanikiwa kuwa timu ya kwanza kukata tiketi ya kucheza nusu fainali ya First League hatua ya Nane Bora baada ya kushinda mchezo wake wa pili dhidi ya Cosmopolitan ya Dar kwa bao moja.

Mkwaju wa penati uliopigwa na Tungu Robert dakika ya 72 ulitosha kuihakikishia Stand nafasi ya kucheza nusu fainali huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi dhidi ya Lipuli ya Iringa utakaochezwa Aprili 28.

Ligi hiyo itaendelea tena Aprili 27 kwa michezo miwili Kati ya Dar City ya Dar na Rhino Rangers ya Tabora saa 10:00 alasiri na TMA Stars ya Arusha itakua mwenyeji wa African Lyon ya Dar saa 1:00 usiku.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *