DAR CITY MAMBO SAFI, TMA IKIENDELEA KUTAMBA

TIMU ya Dar City kutoka Mkoani Dar es Salaam imefanikiwa kushinda mchezo wa kwanza katika mashindano ya First League hatua ya Nane Bora dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora kwa mabao 2-1.

Dar City iliyopata suluhu mchezo wa kwanza dhidi ya TMA FC ya Arusha imekwea mpaka nafasi ya kwanza katika msimamo wa kundi B baada ya kufikisha alama nne huku mabao yake katika mchezo wa leo yakifungwa na Nassoro Kondo na Said Dunia huku bao pekee la Rhino likifungwa na Ramadhan Athuman.

Rhino Rangers italazimika kupata ushindi katika mchezo wa mwisho dhidi ya TMA Aprili 29 ili kujihakikishia nafasi ya kucheza nusu fainali ya First League hatua ya Nane Bora msimu huu kama ilivyofanya msimu uliopita kwenye mashindano yaliyofanyika mkoani Mwanza.

TMA ya Arusha imeendeleza rekodi yake ya kutokupoteza mchezo wowote wa First League msimu huu baada ya kupata ushindi wa bao moja dhidi ya African Lyon ya Dar.

Timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu kutoka Ligi ya Mabingwa Mkoa imekuwa na rekodi nzuri ikiwa timu iliyofungwa mabao machache mpaka sasa msimu huu (9).

Ligi hiyo itaendelea tena Aprili 28 kwa michezo miwili, Lipuli ya Iringa itakuwa mwenyeji wa Stand United ya Shinyanga saa 10:00 alasiri na Alliance ya Mwanza itacheza saa 1:00 usiku na Cosmopolitan ya Dar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *