HAWA HAPA MIAMBA WA NUSU FAINALI NANE BORA

TIMU za Dar City na TMA Stars zimeungana na Cosmopolitan na Stand United katika nusu fainali ya First League hatua ya Nane Bora msimu wa 2022/23.

Dar City ilitoka suluhu dhidi ya African Lyon kwenye mchezo uliopigwa mapema saa 10:00 alasiri na kufikisha alama tano zilizowafanya kumaliza vinara wa kundi B kwa mabao mengi ya kufunga (mawili).

TMA FC ambayo mpaka sasa haijapoteza mchezo wowote wa First League imemaliza nafasi ya pili katika kundi hilo ikiwa na alama tano sawa na Dar City ikizidiwa tofauti ya mabao ya kufunga baada ya kufanikiwa kupata bao moja kwenye mchezo dhidi ya African Lyon.

Baada ya matokeo hayo timu ya Dar City itacheza dhidi ya Cosmopolitan iliyomaliza nafasi ya pili katika kundi A huku TMA ikicheza dhidi ya Stand United iliyomaliza kinara wa kundi A.

Michezo hiyo ya nusu fainali inatarajiwa kupigwa Mei Mosi ambapo Stand United itaikaribisha TMA katika mchezo wa mapema saa 9:00 alasiri huku Dar City ikicheza na Cosmopolitan saa 1:00 usiku.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *