TAKWIMU: FAINALI YA KISASI NANE BORA

FAINALI ya First League hatua ya Nane Bora inatarajiwa kuchezwa Mei 3, kwenye uwanja wa Azam, Dar es Salaam kati ya Stand United ya Shinyanga na Cosmopolitan ya Dar.

Timu hizi zilikutana hatua ya makundi katika mchezo ambao Stand ilishinda kwa bao moja lililofungwa na Tungu Robert dakika ya 70 kwa mkwaju wa penati.

Timu ya Stand mpaka sasa haijapoteza mchezo wowote ikiwa imecheza michezo minne katika hatua ya nane bora ikishinda miwili na kutoka sare miwili.

Huku timu ya Cosmopolitan ikicheza michezo minne pia ikishinda miwili, kutoka sare mmoja na kufungwa mchezo mmoja pekee dhidi ya wapinzani wao wa fainali Stand.

Stand imefanikiwa kufunga mabao matano na kuruhusu mabao mawili ya kufungwa huku Cosmo ikifunga mabao saba na kuruhusu mabao matano ya kufungwa.

Fainali hiyo itatanguliwa na mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu saa 9:00 alasiri kati ya Dar City iliyofungwa na Cosmopolitan na TMA FC iliyopoteza mchezo wake wa kwanza wa First League hatua ya nane bora dhidi ya Stand siku ya Mei Mosi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *