TIMU ya Yanga inayoshika nafasi ya kwanza katika Ligi Kuu ya NBC mpaka mzunguko wa 27 imeendeleza rekodi nzuri ya kushinda mechi katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuifunga Marumo Gallants ya Afrika Kusini mabao 2-0.
Mabao yaliyofungwa na mchezaji wa kimataifa wa Burkina Faso Stephane Aziz Ki na Bernard Morrison wa Ghana yameiweka Yanga nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya fainali katika michuano hiyo.
Yanga imekuwa na rekodi ya kushinda michezo ya Kimataifa kwa asilimia 100 msimu huu ikishinda michezo yote iliyocheza uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Timu hiyo itatupa karata yake ya pili dhidi ya Marumo nchini Afrika Kusini Mei 17 katika uwanja wa Peter Mokaba kwenye Mji wa Polokwane.
Katika mchezo huo wa marudiano Yanga inahitaji ushindi au sare ili kufuzu hatua ya Fainali kwa mara ya kwa katika historia ya timu hiyo kwenye ngazi ya kimataifa.