MZUNGUKO wa tatu wa Ligi Kuu ya NBC unatarajiwa kutamatika leo kwa michezo miwili kupigwa kwenye viwanja viwili tofauti vya mkoa wa Dar es Salaam.
Saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Uhuru, Dar timu ya Simba iliyoshinda michezo yote miwili mpaka sasa itakuwa mwenyeji wa Coastal Union ya Tanga ambayo bado haijapata ushindi katika mchezo wowote wa ligi msimu huu.
Timu ya Azam itakua mwenyeji wa Singida BS saa 1:00 usiku kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar ikiwa ni mchezo wa mwisho kuchezwa kwenye mzunguko wa tatu.
Azam inacheza na Singida huku ikiwa na rekodi ya kushinda michezo yote kwenye uwanja wa nyumbani huku Singida ikiwa haijapata ushindi wala kufunga bao kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu.