MCHEZAJI wa Young Africans raia wa Tanzania Clement Mzize ameendelea kuwa ‘Mwiba’ kwa mabeki wa timu pinzani baada ya kufanikiwa kufunga jumla ya mabao 13 hadi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC.
Mzize amefunga idadi hiyo ya mabao huku timu yake ikisalia na michezo minne kutamatika kwa msimu wa 2024/25.
Prince Dube wa Young Africans na Jean Ahoua wa Simba wanafuata nyuma ya Mzize wakifunga mabao 12 kila mmoja huku Ahoua akifunga mikwaju ya penati mitano hadi sasa na kuwa kinara wa kufunga mabao kwa penati.
Jonathan Sowah anafuatia akifunga jumla ya mabao 11 huku akiwa amecheza michezo tisa pekee baada ya kujiunga na timu yake kwenye dirisha dogo la usajili.
Elvis Rupia wa timu ya singida Black Stars anafuata nyuma ya mshambuliaji mwenzake wa timu ya Singida Jonaathan Sowah akiwa na mabao kumi.