Category: STORY

CLATOUS CHAMA NA REKODI MPYA LIGI KUU YA NBC.

 

‘STAA’ wa Simba, Clatous Chama ameendelea kuandika historia ndani ya LIGI KUU NBC baada ya kuwa mchezaji wa kwanza kushinda tuzo ya Mchezaji bora wa mchezo(Man of the Match) mara nne mfululizo katika msimu wa 2025/2026.

Kiungo huyo raia wa Zambia ameonyesha kiwango cha juu katika mechi za hivi karibuni, akiongoza safu ya ushambuliaji ya Simba kwa pasi za mwisho, mabao muhimu na uwezo wake wa kutawala mchezo katikati ya uwanja.

Chama alianza mfululizo huo kwenye Kariakoo Derby kati ya Young Africans na Simba iliyomalizika kwa sare ya mabao 2-2, ambapo alionyesha kiwango bora na kuwa mhimili mkubwa wa Simba katika mchezo huo mkubwa wa watani wa jadi.

Baada ya derby hiyo, aliendelea kung’ara katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Tanzania Prisons, kabla ya kuiongoza Simba kushinda 1-0 dhidi ya JKT Tanzania na alikuwa nyota katika ushindi mwingine wa mabao 3-0 dhidi ya Mashujaa FC.

Katika mechi zote nne, Chama aliondoka na tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi, jambo lililoonyesha ubora wake wa kipekee na mchango mkubwa ndani ya kikosi cha Simba msimu huu.

Ubora wa Chama umeendelea kuwa silaha muhimu kwa Simba katika mbio za ushindi, huku mashabiki wakizidi kuvutiwa na mchango wake kila anapoingia uwanjani.

Uchezaji wake wa kujiamini, uzoefu na uwezo vimemfanya kuwa mmoja wa nyota wanaong’ara zaidi kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu.

MZUNGUKO WA 23 WATAMATIKA KIBABE LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC jana ilitoa burudani ya kiwango cha juu huku mashabiki wakishuhudia jumla ya mabao 13 yakifungwa kwenye viwanja tofauti.

Mchezo wa mapema kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya uliwakutanisha ‘Maafande’ wa Tanzania Prisons waliopata ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Fountain Gate kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.

George Mpole aliibeba timu hiyo kwa bao lake la dakika ya 26 lililowapa furaha mashabiki wa nyumbani huku Fountain ikipambana kusawazisha lakini ukuta wa Prisons ulikuwa imara mpaka filimbi ya mwisho.

Mchezo mwingine wa mapema uliotikisa zaidi jana ulikuwa kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya KMC ambapo mashabiki walishuhudia tamasha la mabao saba baada ya Mtibwa kuibuka na ushindi wa 4-3 kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Magata Fredrick alianza mapema dakika ya 30 kabla ya Oscar Masai, Said Mkopi na Kassimu Msafiri kuongeza mabao mengine yaliyowapa ushindi muhimu huku kwa upande wa KMC, Daruweshi Saliboko alipachika mawili na Rashid Chambo akiingia kwenye orodha ya wafungaji ingawa juhudi zao hazikutosha kuzuia kipigo hicho.

Kwenye uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma timu ya Simba imeendelea kuonyesha makali yake baada ya kuichapa Mashujaa mabao 3-0 kwenye mchezo uliokuwa na ‘presha’ kubwa.

Nahodha Clatous Chama alikuwa nyota wa mchezo huo baada ya kufunga mabao mawili dakika za 6 na 79 kabla ya Seleman Mwalimu aliyeingia kipindi cha pili kuweka msumari wa mwisho dakika ya 90+2.

Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha alama 52 na kuendelea kuweka presha kubwa kwenye mbio za ubingwa wakiwasogelea kwa karibu wapinzani wao wakubwa Young Africans waliopoteza mchezo wao uliopita dhidi ya Dodoma Jiji waliokusanya alama 54.

Mchezo wa mwisho ulishuhudia Azam ikipata ushindi wa dakika za mwisho baada ya kushinda 2-0 dhidi ya Pamba Jiji ya Mwanza.

Feisal Salum aliipatia Azam bao la kwanza dakika ya 90 linalomfanya kufikisha mabao 11 na kuendelea kuwa kinara wa mabao kwenye Ligi Kuu ya NBC hadi sasa huku bao la pili likifungwa na Jephte Kitambala.

Matokeo hayo yanaendelea kuongeza moto kwenye msimamo wa ligi huku kila timu ikipigania malengo yake kama vile ubingwa, nafasi za kimataifa na kujiokoa kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja.

LIGI KUU YA NBC KUPAMBA MOTO LEO.

 

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo minne muhimu itakayochezwa ikiwa ni muendelezo wa mzunguko wa 23 katika viwanja tofauti huku kila timu ikisaka alama muhimu kuelekea mwisho wa msimu.

Timu za juu zinapigania ubingwa huku zile za chini zikihangaika kujinasua kwenye hatari ya kushuka daraja na kucheza Ligi ya Championship ya NBC.

Mchezo wa kwanza utawakutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya KMC katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro Majira ya saa nane mchana ambapo Mtibwa Sugar wanaingia wakiwa nafasi ya 11 kwenye msimamo huku KMC wakiwa nafasi ya mwisho.

Katika mchezo mwingine Tanzania Prisons watawakaribisha Fountai Gate kwenye uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya majira ya saa nane mchana katika pambano litakalokuwa na ushindani mkubwa.

Tanzania Prisons wanashika nafasi ya 15 huku Fountain Gate wakiwa nafasi ya 10 na alama 25 wakisaka kuendelea kubaki kwenye nafasi za juu za msimamo ili kuepuka kushuka daraja.

Mashujaa watakuwa na kazi ngumu dhidi ya timu ya Simba inayosaka taji la Ligi Kuu ya NBC baada ya misimu minne huku Mashujaa ikiwa nafasi ya tisa kwenye msimamo ikipambana kujihakikishia nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu ujao.

Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma majira ya saa 10 :15 jioni na unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora wa timu zote mbili msimu huu.

Katika mchezo mwingine wa kusisimua Azam FC watachuana na Pamba Jiji Katika uwanja wa Azam complex jijini Dar es salaam majira ya saa 12:30 jioni.

Azam wanaingia wakiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo huku Pamba Jiji wakiwa nafasi ya saba, kila mmoja akihitaji ushindi ili kutimiza malengo yake msimu huu.

DODOMA YAISIMAMISHA YOUNG AFRICANS, COASTAL IKIILIZA MBEYA CITY.

TIMU ya Dodoma Jiji imemaliza utemi wa timu ya Young Africans wa kucheza michezo zaidi ya 40 bila kufungwa katika Ligi Kuu ya NBC baada ya kuifunga 3-2 kwenye uwanja wa Airtel Stadium, Singida huku timu ya Mbeya City ikikubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa timu ya Coastal Union.

Dakika mbili zilimtosha kiungo wa Young Africans,Allan Okello kufungua ukurasa wa mabao kwa kuitanguliza Young Africans lililodumu kwa dakika 27 kabla ya beki wa wababe hao wa Kariakoo Bakari Mwamunyeto kujifunga na kufanya ubao usome 1-1 kabla ya Okello kurejea tena nyavuni dakika ya 41 na kufanya mchezo huo kwenda mapumziko ‘Wananchi’ wakiongoza 1-2.

Kipindi cha pili Dodoma Jiji walirejea kwa kasi kubwa ikiwa azma yao kubwa n kuhakikisha alama zinabaki nyumbani na dakika ya 89 Mwana Kibuta alifunga bao la pili kwa Dodoma kabla ya Waziri Junior kupeleka kilio ‘Jangwani’ kwa bao la tatu ndani ya dakika za nyongeza hivyo mchezo kuisha kwa matokeo ya 3-2.

Young Africans imesalia kileleni ikiwa na alama 54 huku Dodoma Jiji ikipanda nafasi ya saba na alama 32.

Mchezo mwingine wa mapema ulichezwa uwanja wa Sokoine jijini Mbeya ambapo Mbeya City iliikaribisha timu ya Coastal Union ya Tanga mchezo na kushuhudia ‘Wagosi wa kaya’ wakiondoka na alama zote tatu baada ya ushindi wa mabao 2-0.

Ilimchuka dakika 35 mshambuliaji wa Coastal Maabad Maabad kufungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati hivyo kwenda mapumziko wakiongoza na kujitengenezea nafasi nzuri kwao kujinasua kutoka nafasi za chini ya msimamo.

Kipindi cha pili dakika ya 74 Saad Mwanza aliiongezea bao la pili Coastal hivyo mchezo kumalizika wakiwa kifua mbele kwa mabao mawili na alama zote tatu.

Matokeo hayo yanaiweka Coastal nafasi ya 11 na alama 25 huku Mbeya City ikiwa nafasi ya 13 na alama 21 ikiwa ni nafasi ya timu zinazocheza mtoano wa kusalia Ligi Kuu ya NBC.

OKELLO,GONCALVES WANG’ARA TUZO ZA TFF APRIL

Kiungo mshambuliaji wa Young Africans, ALLAN OKELLO, amechaguliwa kuwa MchezajiBora wa mwezi Aprili wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/26, huku PEDRO GONCALVES wa Young Africans, akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Okello alionesha kiwango kizuri chenye mwendelezo akiwashinda Pacome Zouzoua waYanga na Idd Selemani wa Azam FC, alioingia nao fainali katika mchakato wa tuzo zamwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mchezaji huyo alitoa mchango mkubwa kwa timu yake katika michezo mitatu aliyochezamwezi huo, akifunga bao moja na kuhusika na mengine sita kwa dakika 320 alizocheza.

Kwa upande wa Pedro aliyeingia fainali na Steve Barker wa Simba na Etiene Ndairagijewa TRA United, aliiongoza Young Africans kushinda michezo yote mitatu iliyochezamwezi huo na kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi, ikifunga mabao 12 nahaikuruhusu bao. Young Africans ilizifunga Tanzania Prisons (3-0), Mbeya City (6-0) naPamba Jiji (0-3).

Wakati huohuo Kamati ya Tuzo, imemchagua HASSAN MWATEREMA wa Kagera Sugar kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Aprili wa Ligi ya Championship ya NBC 2025/26, hukuJUMA KASEJA pia wa Kagera Sugar akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Mwaterema aliyeingia fainali na Japhet Mayungu wa TMA na Salum Mlemwa wa Gunners, alionesha kiwango chenye mwendelezo, ikiwa ni pamoja na kufunga mabao mawili kwadakika 139 za michezo miwili aliyocheza.

Kwa upande wa Kaseja aliyeingia fainali na Zuberi Katwila wa Geita Gold na MbwanaMakata wa Polisi Tanzania, aliiongoza timu yake kushinda michezo yote miwili iliyochezamwezi huo ikiendelea kubaki nafasi ya pili.

Pia Kamati ya Tuzo imeteua MAGOLI MATATU BORA ambayo yatapigiwa kura namashabiki ili kupata goli bora la mwezi la mashabiki. Magoli hayo ni Pacome Zouzoua(Young Africans vs Mbeya City dakika ya 43), Idd Kipagwile (Dodoma vs Fountain Gate dakika ya 68) na Grayson Gwalala (Coastal v Dodoma Jiji dakika ya 14).