Ligi Kuu ya NBC imeendelea leo Septemba 21 kwa michezo miwili kuchezwa katika viwanja viwili na kushuhudiwa Simba wakiifunga Coastal Union ya Tanga mabao 3-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Uhuru mkoani Dar es salaam.
Mabao yote matatu ya Simba yamefungwa na mchezaji Jean Baleke huku akiingia katika rekodi ya kuwa mchezaji wa pili kufunga mabao matatu kwenye mchezo mmoja ‘Hat-trick’ katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 sambamba na Feisal Salum aliyefunga idadi hiyo ya mabao dhidi ya Tabora United.
Azam FC waliwaalika Singida BS katika uwanja wa Azam Complex na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 yaliyofungwa na Cheikh Sidibe na Iddi Selemani ‘Nado’ huku la Singida BS likifungwa na Marouf Tchakei.
Ligi hiyo itaendelea tena Septemba 29 kwa michezo miwili kuchezwa Kati ya JKT Tanzania na Kagera Sugar wakati mchezo wa pili Coastal Union watawaalika Tabora United.