TANZANIA YAANZA NA USHINDI CHAN 2024.

TANZANIA YAANZA NA USHINDI CHAN 2024.

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imeanza vyema michuano ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza Ligi za ndani CHAN 2024 kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Timu ya Taifa ya Burkina Faso.

Mabao ya Stars yalifungwa na Abdul Suleimani anaekipiga kwenye timu ya Azam ya Dar es Salaam kwa mkwaju wa penati huku la pili likifungwa na Mohammed Hussein aliyemaliza mkataba wake na timu ya Simba akimaliza kazi safi iliyofanywa na Iddy Selemani (Nado) wa Azam.

Mchezo huo ulitanguliwa na Shamra shamra za ufunguzi wa michuano hiyo ambao kwa upande wa burudani ziliongozwa na msanii wa Bongo Fleva Raymond Mwakyusa maarufu Kama ‘Rayvanny’.

Timu ya Tanzania inaundwa na ‘mastaa’ mbalimbali wanaocheza Ligi za ndani ikiwemo Ligi Kuu ya NBC na Ligi ya Championship ya NBC.

Tanzania itarejea tena uwanjani Jumatano ya Agosti 6, saa 2:00 usiku ikiivaa timu ya Taifa ya Mauritania.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *