DODOMA, PWANI, SHINYANGA NBC CHAMPIONSHIP INAPIGWA LEO.

 

NBC Championship mzunguko wa 21 inaendelea leo kwa michezo mitatu kuchezwa kwenye MIKOA ya Dodoma, Pwani na Shinyanga.

Mkoani Dodoma Ruvu Shooting itakuwa mwenyeji wa Mbuni saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Jamhuri.

Ruvu Shooting ipo nafasi ya mwisho kwenye msimamo na alama nne huku Mbuni ikiwa nafasi ya sita na alama 37.

Mkoani Pwani Green warriors itaialika Pamba kwenye uwanja wa mabatini saa 10:00 alasiri, Green warriors inashika nafasi ya 11 na alama 20 huku Pamba ikiwa nafasi ya pili na alama 43.

Mchezo wa mwisho kwa leo utazikutanisha Stand United dhidi ya Polisi Tanzania saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *