FOUNTAIN ‘HALI TETE’ LIGI KUU YA NBC.

 

Ligi Kuu ya NBC imeendelea mzunguko wa 28 JKT Tanzania ikiikaribisha Fountain Gate ya mkoani Manyara kwenye uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo na ‘kuichapa’ mabao 3-1 na kuishusha hadi nafasi ya 13 ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Ilimchukua dakika saba pekee Mohamed Bakari kuwaamsha mashabiki wa JKT kwa kuipatia timu yake bao la kwanza baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Edward Songo.

Shiza Kichuya aliipatia JKT bao la pili dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza (45) na ‘Maafande’ kwenda mapumziko wakiongoza 2-0.

Edward Songo alipigilia ‘Msumari’ wa tatu dakika ya 60 na kuifanya Fountain kuwa timu iliyofungwa mabao mengi hadi sasa (54).

Dakika ya 86 Fountain Gate ‘Walijipata’ na kufunga bao la kwanza kupitia kwa William Edger hivyo mchezo kumalizika 3-1.

Fountain iliyoanza vyema
Msimu huu wa Ligi Kuu ya NBC imejikuta na muendelezo mbovu wa matokeo mazuri ikiwa miongoni mwa timu zilizopoteza michezo mingi (15) nyuma ya Kagera Sugar (16) na Ken Gold (17) zilizoshuka daraja.

Shiza Kichuya wa JKT aliibuka mchezaji bora baada ya kufunga bao na kutoa pasi ya bao hivyo kuifanya JKT kufikisha alama 35 na kukwea hadi nafasi ya sita ya msimamo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *