HAWA HAPA NYOTA WAPYA LIGI KUU YA NBC.

DIRISHA la usajili msimu mpya wa 2023/24 kwa klabu za Ligi Kuu ya NBC, Championship, First League na Ligi Kuu ya Wanawake lilifunguliwa Julai Mosi ili kuruhusu timu kuhamisha wachezaji kutoka timu moja Kwenda nyingine.
 
Timu mbali mbali za Ligi Kuu zimeendelea kujiimarisha kwa kutangaza wachezaji na makocha watakaowasimamia katika michezo yao kuelekea msimu mpya.
 
Zifuatazo ni sajili mbalimbali zilizokwisha kutangazwa na  timu za Ligi Kuu ya NBC;
 
SIMBA-  Che Malone Fondoh (Beki)
               Esomba Onana (Mshambuliaji)
               Aubin Kramo (Winga)
                Mikael Igendia (Meneja wa timu)
               Corneille Hategekimana (Kocha wa viungo)
 
YANGA- Miguel Gamondi (Kocha mkuu)
               Nickson Kibabage (Beki)
 
AZAM- Djibril Sillah (Kiungo)
             Feisal Salum (Kiungo)
             Khalifa Ababakar Fall (Kocha wa makipa)
             Ibrahim Diop (Mchambuzi wa mechi kwa njia ya video)
             Allasane Diao (Mshambuliaji)
              Cheikh Sidibe (Beki)
             Bruno Ferry (Kocha msaidizi)
              Jean- Laurent Geronimi (Kocha wa viungo)
 
SINGIDA FOUNTAIN GATE – Yahya Mbegu (Beki)
 
NAMUNGO- Erasto Nyoni (Kiungo)

Timu nyingine 11 zilizosalia bado hazijatangaza usajili wowote huku dirisha likitarajiwa kufungwa Agosti 31.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *