LIGI Kuu ya NBC inarejea juni 18 ikiwa ni mzunguko wa 29 huku michezo yote hiyo itakayochezwa viwanja mbali mbali ikitarajiwa kuanza saa 10:00 alasiri.
Mchezo wa kwanza utachezwa uwanja wa CCM kirumba Pamba Jiji inayotafuta uhakika wa kusalia Ligi Kuu ya NBC itaikaribisha timu ya JKT Tanzania, huku Namungo ikiikaribisha Kagera Sugar iliyoshuka daraja katika uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi.
Timu ya Dodoma Jiji itakuwa mwenyeji wa timu ya Singida Black Stars katika uwanja wa Jamhuri Dodoma na Mashujaa itaialika KMC katika uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.
Kwa upande wa KenGold iliyoshuka daraja itakuwa mwenyeji wa timu ya Simba inayowania ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora huku Tanzania Prisons ikiialika timu ya Young Africans katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
Azam itakuwa mwenyeji wa Tabora United katika uwanja wa Azam Complex uliopo jijini Dar es Salaam na mchezo wa mwisho utakuwa kati ya Coastal Union na Fountain Gate katika uwanja wa Mkwakwani uliopo mkoani Tanga.