RATIBA ZA MASHINDANO ZATAMBULISHWA.

BODI ya Ligi Kuu Tanzania imetangaza tarehe za matukio yote ya msimu mpya wa 2023/24 ikiwa ni pamoja na siku za kuanza kwa Ligi Kuu ya NBC, Championship na First League.

Ligi Kuu ya NBC inatarajiwa kuanza Agosti 15 ikitanguliwa na michezo ya Ngao ya Jamii itakayochezwa mkoani Tanga kuanzia Agosti 9 mpaka Agosti 13 .

Ligi ya Championship iliyopokea timu tatu ngeni za TMA Stars, Cosmopolitan na Stand United kutoka ligi ya First League inatarajiwa kuanza Septemba 2 ikiwa ni siku 17 baada ya kuanza kwa Ligi Kuu ya NBC.

Ligi ya First League inatarajiwa kuanza Oktoba 21 huku hatua ya Nane Bora ya ligi hiyo ikitarajiwa kuanza Aprili 10.

Michezo ya Ligi Kuu ya NBC itakua mbashara kupitia chaneli za Azam huku ikisikika kwa njia ya redio kupitia kituo cha TBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *