MICHEZO mitatu ya Ligi ya NBC Championship mzunguko wa 21 imechezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.
Ruvu Shooting kwa mara ya kwanza ndani ya NBC Championship inaondoka na alama tatu baada ya kuifunga Mbuni mabao 2-1 kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma mchezo uliopigwa saa 8:00 mchana, Ruvu Shooting imewachukua michezo 21 kusubiri alama tatu za kwanza ndani ya Ligi ya NBC Championship.
Mkoani Pwani kwenye uwanja wa Mabatini saa 10:00 alasiri Green Warriors ikaialika Pamba na mchezo huo kumalizika kwa suluhu.
Mchezo wa mwisho kwa leo ukazikutanisha Stand United dhidi ya Polisi Tanzania kwenye uwanja wa Mwadui Complex na kumalizika kwa Polisi Tanzania kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.