TIMU ya Simba imeanza msimu wa Ligi Kuu ya NBC 2023/24 kibabe ikiwa haijafungwa wala kutoa sare mchezo wowote mpaka mzunguko wa tano kukamilika.
Simba imeshinda michezo miwili nyumbani dhidi ya Dodoma Jiji kwa mabao 2-0 na Coastal Union mabao 3-0 huku ikishinda michezo mitatu ya ugenini dhidi ya Mtibwa Sugar mabao 2-4, 1-3 dhidi ya Tanzania Prisons, 1-2 dhidi ya Singida BS.
Simba inaongoza msimamo wa Ligi Kuu ya NBC huku ikishika nafasi ya pili kwa kufunga mabao (14) nyuma ya timu ya Yanga yenye mabao (15).