Tag: #NBCPL#STORY

TABORA UTD YATAMBA

Mkoani Tabora Tanzania Prisons imepoteza mchezo wa pili mfululizo dhidi ya Tabora United kwa mabao 3-1.

Tabora UTD iliyopoteza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Azam kwa mabao 4-0 imepata ushindi huo wa kwanza kwa mabao ya John Ben aliefunga mawili na Erick Okutu huku bao la Prisons likifungwa na Samson Mbangula.

Prisons imeruhusu mabao sita kwenye michezo miwili iliyopita huku wakiwa na alama moja pekee waliyopata suluhu dhidi ya Singida Fountain Gate inayowaweka nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

KIVUMBI CHA LIGI KUU YA NBC KUANZA LEO

Pazia la Ligi kuu ya NBC msimu wa 2022/2023 linafunguliwa rasmi  hii leo Agosti 15, 2022 kwa timu nne za Ihefu SC, Ruvu Shooting FC, Namungo FC na Mtibwa Sugar FC  kushuka katika viwanja viwili kuzisaka alama tatu.

Mchezo wa kwanza wa ufunguzi utazikutanisha Ihefu  dhidi ya Ruvu Shooting majira ya saa 10:00 alasiri katika dimba la Highland Estate, Mbarali  Mkoani Mbeya wakati mchezo wa pili utazikutanisha  Namungo dhidi ya Mtibwa Sugar katika dimba la Benjamin Mkapa kuanzia saa 1:00 usiku.

Timu ya Namungo  inatumia uwanja wa Benjamin Mkapa kama uwanja wake wa nyumbani baada ya uwanja wao wa Majaliwa, Lindi kuwa  katika maboresho.

Msimu huu wa 2022/2023 unashirikisha jumla ya timu 16 ambapo kila timu itacheza jumla ya michezo 30 kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na  kufanya jumla ya  michezo 240 sawa na michezo 120 nyumbani na 120 ugenini kwa timu zote.