Mkoani Tabora Tanzania Prisons imepoteza mchezo wa pili mfululizo dhidi ya Tabora United kwa mabao 3-1.
Tabora UTD iliyopoteza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Azam kwa mabao 4-0 imepata ushindi huo wa kwanza kwa mabao ya John Ben aliefunga mawili na Erick Okutu huku bao la Prisons likifungwa na Samson Mbangula.
Prisons imeruhusu mabao sita kwenye michezo miwili iliyopita huku wakiwa na alama moja pekee waliyopata suluhu dhidi ya Singida Fountain Gate inayowaweka nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.