TANZANIA KUIVAA MOROCCO ROBO FAINALI CHAN.

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ itaivaa timu ya Taifa ya Morroco kwenye hatua ya Robo Fainali ya michuano ya CHAN 2024 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Agosti 22, 2025. 

Taifa Stars ilifika hatua hiyo baada ya kuongoza kundi B ikiwa na alama 10 baada ya kushinda michezo mitatu na kupata sare mchezo mmoja huku ikifunga jumla ya mabao matano na kuruhusu bao moja pekee.

Kwa upande wa Morocco ilifikia hatua hii baada ya kushika nafasi ya pili kwenye kundi A lililoongozwa na Taifa jirani la Kenya.

Morroco ilishinda michezo mitatu na kupoteza mchezo mmoja hivyo kumaliza kwenye nafasi ya pili ikiwa na alama tisa.

Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufika hatua ya Robo Fainali ya michuano ya CHAN kwenye historia ya ushiriki wake kwenye mashindano hayo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *