KARIA AFUNGUA SEMINA YA FIFA KUHUSU WELEDI KATIKA UENDESHAJI KLABU NCHINI.

Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Wallace Karia amefungua semina ya siku mbili iliyoandaliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) jijini Dar es salaam kuhusu weledi katika uendeshaji wa klabu nchini kwa wenyeviti na watendaji wakuu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo Karia amewashukuru timu ya FIFA chini ya Mkuu wa Maendeleo ya Programu wa FIFA, Solomon Mudege kwa kuweka semina hii kwa wenyeviti na watendaji wakuu wa klabu za Ligi Kuu ya NBC.

Karia amesema kuwa uanzishwaji wa program hii kwa klabu hususani namna klabu zitakavyofanya biashara ya mpira kiueledi zaidi na pia wakati wa program hii wataelewa namna ya kushughulikia mipango mikakati ya klabu zao.

Aidha Karia amesema kuwa kama unataka klabu yako kuwa sahihi ndani nje ya uwanja unapaswa kuwa na mpango mkakati maalumu.

Programu hii itazisaidia klabu kubadilisha mtazamo katika kila Nyanja ili kwenda na wakati.

“Naamini baada ya programu hii klabu zetu zitabadili mtazamo kwa upande wa uongozi na mtafanya mambo yote kwa ufanisi mkuu nami sina budi kumshukuru Rais wa FIFA, Gianni Infantino kwa programu hii inayokidhi mazingira yetu ya kiafrika na tunatamani ziwepo nyingi zaidi” amesema Karia.

Karia amemaliza kwa kutoa nukuu maarufu isemayo kuwa malengo bila mpango ni sawa na matamanio hivyo amewaomba washiriki wa program hii kuweza kuwafundisha wenzao katika klabu ili hata kama ikitokea wameondoka wawepo watu kuendeleza mipango mikakati iliyowekwa na klabu.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *