Author: Loveness Bernard

TRA KUIVAA SIMBA, MBEYA CITY WENYEJI WA AZAM.

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo miwili itakayopigwa kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha ambapo timu ya TRA United itaikaribisha timu ya Simba na kwenyw uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara Mbeya City itaialika timu ya Azam.

Michezo hiyo itakayochezwa saa kumi jioni ni muhimu kwa timu zote kutokana na timu hizo kutaka kujiweka nafasi nzuri ya kupambania ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC.

TRA ipo nafasi ya nane katika msimamo ikicheza michezo 17 ushindi sita, sare tano na kufungwa michezo sita huku ikiwa imekusanya alama 23.

Wachezaji wa Simba.

Kwa upande wa Simba iko nafasi ya pili kwenye msimamo ikicheza michezo 16 ushindi mechi 10 sare tano na kufungwa mchezo mmoja huku ikikusanya jumla ya alama 35.

Mchezo wa pili ni muhimu kwa Mbeya City ambapo timu hiyo inatafuta alama iweze kupanda zaidi katika eneo zuri huku Azam ikiwa katika mbio za ubingwa.

wachezaji wa Mbeya city

Mbeya City ipo nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikicheza michezo 17 kushinda michezo minne, sare nne na kufungwa michezo tisa huku ikikusanya alama 16.

Kwa upande wa Azam ipo nafasi ya tatu ikicheza michezo 17 kwa kushinda michezo nane na sare tisa huku ikikusanya alama 33.

IMORO,BARKER WANG’ARA TUZO MACHI

BEKI wa Singida Black Stars, Ibrahim Imoro amechaguliwa kuwa mchezaji Bora wa mwezi Machi wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/26, huku Steve Barker wa Simba akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Imoro alionesha kiwango kizuri chenye mwendelezo kwa mwezi huo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao matatu katika michezo mitano ambayo Singida ilicheza na kuisaidia timu yake kupanda kutoka nafasi ya 10 hadi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

 Beki huyo aliwashinda Anicet Oura wa Simba na Lamine Jarjou wa Singida Black Stars alioingia nao fainali katika mchakato wa Tuzo za Mwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kocha wa Simba Steve Barker

Kwa upande wa Barker aliyeingia fainali na Pedro Goncalves wa Yanga na David Ouma wa Singida Black Stars, aliiongoza timu yake kushinda michezo miwili na kutoka sare miwili na kupanda kutoka nafasi ya tatu hadi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

Wakati huohuo Meneja wa Uwanja wa Airtel mkoani Singida, Omar Malule, amechaguliwa kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Machi kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.

Mchezaji wa Mbuni,Omari Mponda.

Katika hatua nyingine Omari Mponda wa Mbuni amechaguliwa Mchezaji Bora wa Mwezi Machi wa Ligi ya NBC Championship 2025/26, huku Zuberi Katwila wa Geita Gold, akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Mponda aliyeingia fainali na Yusuf Mhilu na Maulid Shaaban wote wa Geita Gold alionesha kiwango chenye mwendelezo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao mawili kwa dakika 155 za michezo miwili aliyotumika mwezi huo.

Kocha wa Geita Gold, Zuberi Katwila.

Kwa upande wa Katwila aliyeingia fainali na Leonard Budeba wa Mbuni na Twaha Beimbaya wa B19, aliiwezesha timu yake kushinda michezo yote miwili iliyocheza na kupanda kutoka nafasi ya pili hadi ya kwanza kwenye msimamo wa ligi.

Pia Kamati ya Tuzo imeteua magoli matatu bora ambayo yatapigiwa kura na mashabiki wa mpira wa miguu nchini, ili kupata Tuzo ya Goli Bora la Mashabiki kwa mwezi Machi.

Magoli hayo ni Prince Dube (Singida v Yanga dakika ya 38), Joseph

Akandwanaho (TRA v Namungo dakika 90+1) na Ibrahim Imoro (Mbeya City v

Singida Black Stars dakika ya 86).

Ratiba ya Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

TAARIFA YA MCHEZO WA TRA DHIDI YA SIMBA.

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) inautaarifu umma kuwa mchezo namba saba (7) wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 (TRA United FC vs Simba SC), utafanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Aprili 9, 2026 kuanzia saa 10:00 alasiri.

Aidha, Bodi inatoa taarifa kuwa mashabiki wote ambao walinunua tiketi kwa ajili ya mchezo huo ambao uliahirishwa Machi 14, 2026 baada ya mvua kubwa kunyesha jijini Arusha na kusababisha uwanja kukosa sifa za kisheria, watatumia tiketi hizo kuingia uwanjani katika mchezo wa Aprili 9, 2026, ambapo shabiki atalazimika kuwa na kadi (N-CARD) ambayo aliitumia kununua tiketi ya mchezo ulioahirishwa, kwa ajili ya uhakiki getini.

Tayari wauzaji wa tiketi za mchezo huo, National Internet Data Center (NIDC) wamerejesha tiketi zote zilizonunuliwa, kwenye kadi za mashabiki hao bila kujali shabiki alikuwa ameshaingia uwanjani ama hakuingia kabisa, na kwamba mashabiki hao hawatapaswa kununua tena tiketi.Tiketi ambazo ziliuzwa katika mchezo huo ni VVIP 95, VIP 567 na Mzunguko 3,215.

Bodi inawakumbusha mashabiki ambao hawakununua tiketi kwenye mchezoulioahirishwa, kuwa tiketi zinapatikana (zinauzwa) kwenye vituo vya N-CARD vya kuuzia tiketi na kupitia mitandao ya simu kwa gharama zifuatazo; VVIP – 50,000, VIP (Wing A & B) – 30,000 na Mzunguko – 10,000

Bodi ya Ligi inawashukuru sana mashabiki wa mpira wa miguu kwa ushirikiano mkubwa wanaoendelea kuutoa kwa Bodi na klabu zake, ikiwemo kununua tiketi na kuingia viwanjani kuziunga mkono klabu zetu.

Imetolewa na;

Idara ya Habari na Mawasiliano

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)

SINGIDA KUIKARIBISHA KMC, PAMBA, YOUNG AFRICANS KUKIPIGA KIRUMBA.

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo miwili itakayopigwa kwenye viwanja vya Airtel mkoani Singida ambapo Singida Black Stars itaialika KMC na CCM Kirumba mkoani Mwanza timu ya Pamba Jiji itaikaribisha timu ya Young Africans.

Wachezaji wa Singida Black Stars wakishangilia.

Michezo hiyo ni muhimu kwa timu zote kutokana na namna Ligi hiyo inavyozidi kupamba moto, Singida Black Stars iliyopo nafasi ya sita inacheza majira ya saa nane mchana huku ikiwa imeshinda michezo saba sare nne na kufungwa michezo sita huku ikikusanya alama 25.

DARUESHI SALIBOKO - KMC
DARUESHI SALIBOKO – KMC

Kwa upande wa KMC inashika nafasi ya mwisho (16) katika msimamo ikicheza michezo 17 na kushinda miwili, sare mbili na kufungwa 13 huku ikikusanya alama 8.

Wachezaji wa Pamba Jiji wakishangilia.

Mchezo wa pili ni muhimu kwa Pamba Jiji ikitaka kuendeleza rekodi ya kutokufungwa mchezo wowote katika uwanja wao wa nyumbani katika michezo tisa timu hiyo imeshinda michezo mitano na sare nne huku Young Africans ikitaka kuendeleza kukusanya alama ili iwe katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC.

Pamba ambayo iPo nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC imecheza michezo 17 ikishinda michezo sita sare nane na kufungwa michezo mitatu huku ikiweza kukusanya alama 26.

Wachezaji wa Young Africans.

Kwa upande wa Young Africans ipo nafasi ya kwanza katika msimamo ikiwa imecheza michezo 17 kushinda michezo 12 na sare tano huku ikiwa imekusanya alama 41.

SIMBA, COASTAL KUONYESHANA UBABE LEO LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC itaendelea tena mkoani Dar es Salaam leo ambapo timu ya Simba itaikaribisha timu ya Coastal Union katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo saa 1:00 usiku.

Kila timu imejiandaa vyema ikizitaka alama zote tatu ili kujiweka katika nafasi nzuri ambapo Simba inataka kujihakikishia iko kwenye mbio za ubingwa huku Coastal Union ikitaka kujiweka katika nafasi nzuri ya kusalia kwenye ligi hiyo msimu ujao.

Wachezaji wa timu ya Simba

Simba inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 14, kushinda michezo tisa sare nne na kupoteza mchezo mmoja na kukusanya alama 31.

Wachezaji wa timu ya Coastal Union.

Kwa upande wa Coastal Union inashika nafasi ya 13 kwenye msimamo ikiwa na alama 15 katika michezo 16 iliyocheza ikishinda michezo mitatu, sare sita na kupoteza michezo saba.