JOTO la nani kwenda Ligi Kuu namba nne kwa ubora barani Afrika Ligi Kuu ya NBC linazidi kupanda huku timu ya Mbeya City ikiongoza kwa upande wa kufunga mabao mengi kuliko timu yoyote katika Ligi ya Championship ya NBC.
Mbeya City wamefanikiwa kufunga mabao 55 katika michezo 27 ambayo timu hiyo imecheza huku ikiwa imeruhusu bao 24 na kukusanya alama 59 ikiwa nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Mtibwa Sugar.
Mtibwa Sugar wanafuatia kwa kufunga mabao ikiwa imefanikiwa kufunga mabao 53 na ikiruhusu mabao 15 katika michezo 27 iliyocheza huku ikiwa imekusanya alama 66 na ikiongoza katika msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC.
Stand United na Geita Gold wote wamefanikiwa kufunga mabao 47 kila timu huku Stand ikiruhusu mabao 23 pamoja na kuvuna alama 58 ikiwa nafasi ya tatu katika msimamo na Geita Gold ikiruhusu mabao 21 wote wakiwa wamecheza michezo 27 katika Ligi hiyo.
Mbeya Kwanza imefanikiwa kufunga mabao 38 baada ya kucheza michezo 27 ikiruhusu nyavu zake kutikiswa mara 24 na ikiwa nafasi ya sita katika mbio za ubingwa wa Ligi hiyo.