MZIZIMA DERBY

NANI KUIBUKA MBABE WA MZIZIMA ‘DERBY’ LEO ?

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Februari 24, 2025 kwa mchezo mmoja wa ‘Derby’ ya Mzizima kati ya Simba SC na Azam FC kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia majira ya saa 1:00 usiku.

Simba inaingia kwenye mchezo huu ikiwa na alama 50 baada ya michezo yake 19 huku ikifunga mabao 41 na kuruhusu sita (6) pekee.

Kwa upande wa Azam FC ina jumla ya alama 43 baada ya michezo 20 ya Ligi Kuu ya NBC ikifunga mabao 29 na kuruhusu tisa (9) pekee.

Mara ya mwisho timu hizi zilikutana Septemba 26, 2024 visiwani Zanzibar, na mchezo huo kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Kila timu imefanya maboresho kwenye kikosi chake katika dirisha dogo la usajili ambapo Simba imemuongeza kikosini Elie Mpanzu huku Azam FC ikiwasajili Zidane Sereri na Landry Zouzou.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *