MZUNGUKO wa 23 wa Ligi ya Championship ya NBC umehitimishwa jana kwa mchezo mmoja kuchezwa katika uwanja wa Karume Mkoani Mara na kushuhudia Biashara United ikiibuka na Ushindi wa Bao 1-0 dhidi ya African Sports.
Licha ya Ushindi huo Biashara United inaendelea kusalia nafasi ya mwisho kwenye msimamo ikifikisha alama saba baada ya michezo 23.
Ikumbukwe Biashara United ilipokwa alama 15 baada ya kushindwa kutokea kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City.
Mtibwa Sugar inaendelea kusalia kileleni licha ya kupoteza kwenye mchezo wake dhidi ya Stand United ikiwa na alama 54 baada ya michezo 23 ikifuatiwa na Mbeya City na Stand United kwa pamoja zikiwa na alama 49 zikipishana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.