Author: Yahaya Abushehe

‘LADHA’ ZA LIGI KUU YA NBC KUREJEA LEO

LIGI Kuu ya NBC inarejea Leo Novemba 22 kwa michezo miwili baada ya kusimama kwa siku 13 kupisha kalenda ya FIFA ya michezo ya kimataifa.

Mchezo wa kwanza utazikutanisha Geita Gold inayoshika nafasi ya 15 ikiwa na alama saba dhidi ya JKT Tanzania inayoshika nafasi ya sita ikiwa na alama 14 katika mchezo utakaoanza saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita.

Mchezo wa mwisho hii leo utazikutanisha Kagera Sugar inayoshika nafasi ya nane ikiwa na alama 12 dhidi ya KMC iliyo na alama 15 kwenye nafasi ya tano, saa 1:00 usiku kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

RUVU KUJIULIZA KWA STAND , MBUNI, POLISI VITA NBC CHAMPIONSHIP LEO

Ligi ya NBC Championship inaendelea leo Novemba 17 kwa michezo miwili kwenye mikoa miwili tofauti.

Mchezo wa saa 8:00 Mchana Stand United watawaalika Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga.

Stand ipo nafasi ya 10 kwenye msimamo ikicheza jumla ya michezo 10 na kupata ushindi kwenye michezo mitatu, sare tatu na kufungwa minne huku ikikusanya alama 12.

Ruvu Shooting ipo nafasi ya mwisho kwenye msimamo baada ya kucheza jumla ya michezo 10 ikifungwa michezo 9 na kupata sare mchezo mmoja ikiwa haijashinda mchezo wowote na kuwa na alama moja.

Mchezo wa pili utazikutanisha Mbuni dhidi ya Polisi Tanzania saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Black Rhino, Karatu.

Mbuni ipo nafasi ya nne ya Msimamo baada ya kucheza michezo 10 na kushinda mitano wakitoa sare mitatu na kufungwa miwili huku wakikusanya Alama 18 na Polisi wakishika nafasi ya sita kwenye msimamo ikicheza jumla ya michezo 10 ikitoa sare michezo miwili na kufungwa michezo mitatu na kuwa na jumla ya alama 17.

TMA WABABE WA FIRST LEAGUE WANAOTESA NBC CHAMPIONSHIP.

 

Timu ya TMA yenye maskani yake Arusha inayoshiriki ligi ya NBC Championship imekua na mwanzo mzuri ndani ya ligi hiyo hadi hivi sasa huku ikishiriki ligi hiyo kwa msimu wa kwanza.

TMA ndio timu pekee kwenye Ligi ya NBC Championship ambayo haijapoteza mchezo wowote wa ligi hiyo hadi sasa.

Timu hiyo ambayo imepanda daraja msimu huu kutoka First League imekuwa na mwenendo mzuri baada ya kucheza jumla ya michezo tisa ikishinda michezo sita na kwenda sare michezo mitatu.

MASHUJAA, GEITA KUSAKA HESHIMA LIGI KUU NBC

LIGI KUU ya NBC inaendelea leo Novemba 6 kwa michezo miwili kwenye Mikoa miwili tofauti kati ya Mashujaa wakiwaalika Singida BS kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mkoani kigoma na Geita Gold dhidi ya Tabora United kwenye uwanja wa Nyankumbu, Geita huku michezo yote ikianza saa 10:00 alasiri.

Mashujaa wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya Ligi Kuu ya NBC.

Geita Gold inashika nafasi ya 15 kwenye msimamo baada ya kucheza michezo minane ikishinda mmoja, ikisuluhu michezo mitatu na kufungwa mitano hivyo kukusanya alama sita.

Tabora United ipo nafasi ya nane ikishinda michezo miwili,
sare michezo minne na kufungwa mitano hivyo kuwa na alama 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

KMC NDANI YA TATU BORA LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI KUU ya NBC imeendelea Leo kwa Mchezo mmoja katika uwanja wa Uhuru, Dar na kushuhudia KMC akiibuka na Ushindi wa Bao moja dhidi ya Mtibwa Sugar, lililowapeleka mpaka nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Bao pekee na la ushindi kwa KMC limefungwa na Ibrahim Elias Dakika ya 15 ya mchezo na kuifanya KMC kufikisha alama 15 na michezo saba mfululizo bila kupoteza.

Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mitatu, mapema saa 8:00 Mchana Singida BS watawaalika Ihefu katika uwanja wa Liti mkoani Singida, Mashujaa watawaalika Azam FC saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma na Mchezo wa mwisho saa 1:00 usiku Coastal Union watakuwa wenyeji wa Namungo katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.