DIARRA, CAMARA

HUKU DIARRA KULE CAMARA MILANGO IPO SALAMA.

Zimesalia siku nne kuelekea kwenye kwenye ‘DERBY’ ya Kariakoo ambapo Young Africans itakuwa mwenyeji wa Simba kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Machi 8, 2025 kuanzia saa 1:15 usiku.

Young Africans na Simba zinaingia kwenye mchezo huu zikiwa ndio timu zilizoruhusu mabao machache zaidi ya kufungwa, Young Africans ikiruhusu tisa (9) huku Simba ikiruhusu mabao nane (8) pekee.

Moussa Camara wa Simba anaongoza kwa kuwa na hati safi (Cleansheets) akiwa nazo 15 kwenye michezo 20 aliyocheza akitumia jumla ya dakika 1800 huku Djigui Diarra wa Young Africans akifuatia akiwa nazo 11 kwenye michezo 15 aliyoitumikia Young Africans msimu huu akitumia jumla ya dakika 1451.

Ubora wa walinda milango hawa umezifanya timu za Young Africans na Simba kuwa na wastani mdogo wa mabao ya kufungwa hivyo kuufanya mchezo huu wa ‘Derby’ ya kariakoo kuwa na mvuto wa aina yake.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *