TIMU ya Hausung kutoka Makambako mkoani Njombe imekuwa timu ya kwanza kupanda daraja kwenda Ligi ya Championship ya NBC kutoka kundi A la First League.
Hausung wenye alama 25 huku wakiwa wanaongoza kundi A wamefanikiwa kupanda daraja baada ya kucheza michezo 13 kati ya 14 ambayo wanapaswa kucheza.
Mbali na alama hizo Hausung wamefanikiwa kufunga mabao 19 huku wakiruhusu mabao 11 katika michezo 13 huku wakiwa wameshida michezo saba wakitoka sare michezo minne na kufungwa mechi nne.
Nyumbu wapo nafasi ya pili katika msimamo huo wakiwa na alama 21 baaba ya kucheza michezo 13 wakishinda michezo sita,wakipata sare tatu na kufungwa michezo minne huku ukibaki mchezo mmoja ligi hiyo ambao hata kama wakishinda hawataweza kufikia alama ambazo timu ya Hausung imeweza kuzikusanya.