MANUNGU TISHIO KWA TIMU NGENI NBC CHAMPIONSHIP.

UWANJA wa Manungu uliopo Mkoani Morogoro umekuwa tishio kwa timu zinazoenda kucheza dhidi ya mwenyeji wa uwanja huo Mtibwa Sugar baada ya timu hiyo kushinda michezo 12 hadi sasa kwenye uwanja huo na kuwa idadi kubwa hadi sasa kwenye Ligi ya NBC Championship.

Mtibwa iliongeza idadi ya ushindi wikiendi iliyopita baada ya kutoka nyuma dhidi ya Biashara United iliyokuwa ikiongoza 2-0 kipindi cha kwanza na Mtibwa kumaliza mchezo kwa ushindi wa 3-2.

Uwanja wa Kambarage unaotumiwa na Stand United unashika nafasi ya pili baada ya timu mwenyeji wa uwanja huo Stand United kushinda michezo 11 hadi sasa huku idadi hiyo ikitimia baada ya Stand kushinda mchezo uliopita kwa mabao 3-0 dhidi ya African Sports ya Tanga.

Nyankumbu, Geita uwanja unaotumiwa na Geita Gold unafuata baada ya Geita kushinda michezo 11 idadi sawa na Stand inayotumia uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *