USIKU wa deni haukawii kukucha ndivyo unavyoweza kusema, baada ya kusuburi wiki, Siku hatimaye yamesalia masaa kuelekea mchezo wa ‘Derby’ ya Dar es Salaam ambapo Azam FC itaialika Young Africans kwenye uwanja wa Azam Complex kuanzia saa 1:00 usiku.
Mara ya mwisho kukutana kwenye Ligi Kuu ya NBC Young Africans ilikubali kichapo cha bao 0-1 likifungwa na Gibril Sillah kwenye uwanja wa Azam Complex.
Young Africans inaingia kwenye mchezo huu ikiwa kinara wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na jumla ya alama 64 kwenye michezo 24 huku Azam FC ikiwa nafasi ya 3 na alama zake 51.
Viingilio vya mchezo huo ni 10,000 kwa mzunguko, 15,000 kwa VIP B na 20,000 kwa VIP A na zinapatikana kupitia wakala yeyote wa N-Card.
AZAM ALAMA 3 MEZANI