SIMCHIMBA KINARA WA MABAO LIGI YA NBC CHAMPIONSHIP

Ikiwa imesalia michezo mitatu ya Ligi ya Championship ya NBC vita ya ufungaji wa mabao ikiendelea kushika kasi baada ya  mchezaji  wa Geita Gold kutoka mkoani Geita,  Andrew  Simchimba, kuongoza  akiwa ameshatupia mabao  18 katika mechi 20 ambazo amecheza akiwa na timu yake hiyo.

Nafasi ya pili ikishikiliwa na mchezaji Raizin Hafidhi wa Mtibwa Sugar  ya mkoani Morogoro akiwa amefanikiwa kufunga mabao 16, sambamba na mchezaji, Abdulaziz Shahame, wa timu ya TMA ya mkoani Arusha  akiwa na mabao 16

Nafasi ya nne ikichukuliwa na mchezaji  Ambokile Eliud wa Mbeya City  ya mkoani Mbeya akiwa na mabao 9 huku Mwani Ally wa timu hiyo pia akiwa na mabao 9 yanayomfanya kuwa nafasi ya tano.

Mzunguko wa 28  wa Ligi ya NBC Championship utaendelea kesho ambapo mechi zote nane za mzunguko huo zitachezwa majira ya saa kumi jioni.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *