Ikiwa imesalia michezo mitatu ya Ligi ya Championship ya NBC vita ya ufungaji wa mabao ikiendelea kushika kasi baada ya mchezaji wa Geita Gold kutoka mkoani Geita, Andrew Simchimba, kuongoza akiwa ameshatupia mabao 18 katika mechi 20 ambazo amecheza akiwa na timu yake hiyo.
Nafasi ya pili ikishikiliwa na mchezaji Raizin Hafidhi wa Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro akiwa amefanikiwa kufunga mabao 16, sambamba na mchezaji, Abdulaziz Shahame, wa timu ya TMA ya mkoani Arusha akiwa na mabao 16
Nafasi ya nne ikichukuliwa na mchezaji Ambokile Eliud wa Mbeya City ya mkoani Mbeya akiwa na mabao 9 huku Mwani Ally wa timu hiyo pia akiwa na mabao 9 yanayomfanya kuwa nafasi ya tano.
Mzunguko wa 28 wa Ligi ya NBC Championship utaendelea kesho ambapo mechi zote nane za mzunguko huo zitachezwa majira ya saa kumi jioni.