LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja kati ya Tabora United iliyokuwa mwenyeji wa KMC kwenye dimba la Alli Hassan Mwinyi mkoani Tabora saa 10:00 na kumalizika Tabora United kupoteza kwa bao moja.
Deogratius Anthony wa KMC ndiye aliyeibuka shujaa wa KMC kwani bao lake la dakika ya 59 ndio lilipeleka maumivu kwa Tabora na kuifanya KMC kufikisha alama 33 na kupanda kutoka nafasi ya 13 hadi ya 9 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC huku ikisalia michezo miwili kumalizika kwa msimu.
Tabora United imeendeleza rekodi mbaya baada ya kupoteza mchezo wa sita mfululizo kwenye Ligi Kuu ya NBC ikisalia nafasi ya tano na alama 37 mbili zaidi ya JKT inayoshika nafasi ya sita.
Mchezaji wa KMC Deogratius Anthony alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kufunga bao pekee lililoleta utofauti kwenye mchezo huo.