TIMU za Young Africans na Azam zimeanza vyema msimu wa 2025/2026 baada ya kuibuka na ushindi kwenye michezo yao ya kwanza kwenye Ligi Kuu ya NBC iliyochezwa jana Septemba 24, kwenye viwanja vya Benjamin Mkapa na Azam Complex, Dar es Salaam.
Mchezo wa kwanza saa 1:00 usiku uliishuhudia Young Africans ikiikaribisha Pamba Jiji kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa na kuibuka na ushindi wa mabao 3-0.
Mabao ya Young Africans yalifungwa na Lassine Kouma dakika ya 45+4, Bao la pili lilifungwa na mchezaji Maxi Nzengeli dakika ya 63 ya mchezo huku bao la tatu likifungwa na Mudathir Yahya Dakika ya 90+3.

Maxi Nzengeli Nzengeli Alitajwa kama mchezaji bora wa mchezo kutokana na kiwango bora alichoonesha kwenye mchezo huo.
Saa 3:00 usiku Azam FC ilkuwa mwenyeji wa Mbeya City kwenye uwanja wa Azam Complex na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Nassor Saadun ndiye aliyefungua ukurasa wa mabao kwa Azam FC kwenye dakika ya 32 ya mchezo akimalizia krosi safi iliyopigwa na mchezaji Abdul Suleimani ‘Sopu’
Bao la pili la Azam Lilifungwa na dakika ya 46 ya mchezo akimalizia kazi kubwa iliyofanywa na mchezaji mpya wa kikosi hicho Baraket Hmidi.

Ikiwa huo ndio mchezo wake wa kwanza wa kwenye Ligi Kuu ya NBC Baraket Hmidi wa Azam FC Alitajwa kama mcheza bora wa mchezo.
Wanasiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiimba hii tunabeba