SINGIDA BLACK STARS YAPAA KILELENI MSIMAMO WA LIGI KUU YA NBC.

SINGIDA Black Stars imepanda kileleni mwa Msimamo wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao moja dhidi ya Mashujaa kwenye uwanja wa KMC.

Bao pekee la Singida BS limefungwa na mchezaji Elvis Rupia raia wa Kenya dakika ya 45+5 ya mchezo.

Singida Black Stars
Singida Black Stars

Ushindi huo unaifanya Singida BS kufikisha alama sita baada ya michezo miwili huku ikiwa haijaruhusu bao.

Mchezo wa pili ulipigwa saa 10:15 alasiri mkoani Mbeya uliozikutanisha Mbeya City dhidi ya Young Africans kwenye uwanja wa Sokoine na kumalizika kwa Suluhu.

Mbeya City Vs Young Africans
Mbeya City Vs Young Africans

Mchezaji Baraka Filemon  wa Mbeya City alitajwa Kama Mchezaji Bora wa mchezo huo kutokana na mchango mkubwa aliotoa kwa timu yake kwenye mchezo huo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *