YOUNG AFRICANS YAANZA KIBABE 2026.

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya NBC timu ya Young Africans imeanza mwaka 2026 kibabe kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi baada ya kuifunga timu ya Azam FC kwa mikwaju ya penati 5-4.

Mechi hiyo iliyokuwa na upinzani mkali ilishuhudia timu hizo zikitoka suluhu ndani ya dakika 90 huku mchezaji wa Young Africans Pacome Zouzoua wa Young Africans akikosa mkwaju wa penati na Cheickna Diakite wa Azam akishindwa kumaliza mchezo baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.

Young Africans inayoshika nafasi ya pili kwenye maimamo wa Ligi Kuu ya NBC imekuwa timu ya kwanza kushinda kombe kwa mwaka 2026 ikishinda kwa wachezaji wake wote watano kufunga mikwaju yao huku Landry Zouzou akikosa penati yake.

Young Africans imeifunga Azam fainali ya pili mfululizo kwenye ardhi ya visiwa vya Zanzibar baada ya kufanya hivyo kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho iliyopigwa uwanja wa Amaan Complex msimu wa 2024/25 kwa mikwaju ya penati.

 

 

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *