Ratiba ya Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

LIGI KUU YA NBC KUREJEA LEO.

BAADA ya kusimama kwa takribani wiki tano Ligi Kuu ya NBC inatarajiwa kurejea leo Januari 16 kwa mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma kati ya timu ya Dodoma jiji itakayokuwa mwenyeji wa Singida Black Stars.

Dodoma Jiji iliyoanza vibaya msimu huu imeshinda mchezo mmoja pekee wa Ligi Kuu ya NBC kwenye michezo nane iliyocheza huku ikishika nafasi ya 15 kwenye msimamo itaikaribisha Singida Black Stars inayoshika nafasi ya 15 ikishinda michezo miwili baada ya kucheza mitano.

Singida Black Stars inashuka uwanjani leo chini ya kocha mpya David Ouma baada ya kubadilisha majukumu ya aliyekuwa kocha mkuu wa kikosi hicho Miguel Gamondi mwenye nafasi mpya ya Mkurugenzi wa ufundi katika timu hiyo.

Hadi sasa usukani wa Ligi Kuu ya NBC unashikiliwa na timu ya JKT Tanzania yenye alama 17 huku timu ya KMC ikishika nafasi ya mwisho (16) ikikusanya alama nne pekee huku ikiwa imeshinda mchezo mmoja sawa na Dodoma Jiji inayoshika nafasi ya 15.

Mchezo wa leo utapigwa kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma saa 1:00 usiku na ndio mchezo pekee wa Ligi Kuu ya NBC utakaopigwa leo na utarushwa mbashara kwenye chaneli ya Azam Sports.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *