KMC, PRISONS NANI KUMFUNGA PAKA KENGELE LIGI KUU YA NBC?

LIGI Kuu ya NBC inarejea rasmi leo mkoani Dar es Salaam kwa mchezo mmoja baada ya mapumziko mafupi kwa ajili ya michezo ya Kombe la Shirikisho ambapo timu ya KMC itaikaribisha timu ya Tanzania Prisons katika uwanja wa KMC Complex majira ya saa 1:00 usiku.

Mchezo huo ni muhimu kwa timu zote mbili kwani zinatafuta nafasi ya kubaki katika Ligi Kuu ya NBC kutokana na kuwa nafasi mbaya katika msimamo.

KMC iko nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 18 kwa kushinda michezo miwili, sare mbili na kufungwa michezo 14 huku ikiwa imekusanya alama nane tu.

Prisons ipo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 18 kwa kushinda michezo mitatu, sare nne na kupoteza michezo 11 huku ikiwa imekusanya jumla ya alama 13.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *