FOUNTAIN, SIMBA ‘KUKIPIGA’ COASTAL KUIKARIBISHA DODOMA JIJI LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo katika mikoa ya Arusha na Tanga ambapo timu ya Fountain Gate itaikaribisha timu ya Simba katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid huku Coastal ikiikabili Dodoma Jiji katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Mchezo wa kwanza utaanza majira ya saa 10:00 jioni kwa Fountain Gate kuikaribisha timu ya Simba, mchezo huo ukiwa muhimu kwa timu hizo ikiwa ni moja ya kufikia malengo waliyojiwekea.

Fountain Gate iko nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 17 ikishinda michezo minne, sare nne na kufungwa michezo tisa huku ikifanikiwa kukusanya alama 16.

Wachezaji wa Simba.

Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 17 kushinda michezo 10 sare sita na kufungwa mchezo mmoja huku ikiweza kukusanya alama 36.

 

Kwa upande wa mchezo wa Coastal Union utapigwa majira ya saa kumi na mbili jioni ikiwa ni mchezo wa kimbinu kwani kila timu ikizitaka alama zote tatu muhimu ili kusonga mbele ndani ya malengo waliyojiwekea msimu huu.

Coastal Union iko nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 18 ushindi tatu, sare saba na kufungwa michezo nane huku ikiweza kukusanya alama 16.

Wachezaji wa Dodoma Jiji.

Dodoma Jiji ipo nafasi ya nane katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 18 ikiwa imeshinda michezo sita, sare sita na kufungwa michezo sita huku ikiwa imekusanya jumla ya alama 24.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *