MASHUJAA, SINGIDA ‘KUKINUKISHA’, YOUNG AFRICANS, MBEYA CITY VITA YA ALAMA TATU LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo katika mikoa ya Kigoma na Dar es Salaam ambapo timu ya Mashujaa itaikaribisha timu ya Singida Black Stars katika uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma huku Young Africa ikiikabili Mbeya City katika uwanja wa KMC Complex, Dar.

Mchezo wa kwanza utaanza majira ya saa 10:00 alasiri kwa Mashujaa kuikaribisha timu ya Singida Black Stars mchezo huo ukiwa ni muhimu kwa timu hizo ili kufikia malengo waliyojiwekea ya kubeba ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC.

Mashujaa ipo nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 18 ikishinda michezo minne, sare nane na kufungwa michezo sita huku ikifanikiwa kukusanya alama 20.

Wachezaji wa Singida

Singida ipo nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 18 kushinda michezo 8 sare nne na kufungwa michezo sita huku ikikukusanya alama 28.

Kwa upande wa mchezo wa Young Africans na Mbeya City utachezwa majira ya saa 12:30 jioni ikiwa ni mchezo utakaokuwa na upinzani mkali baada ya timu hizo kutoka sare kwenye mchezo wao wa mzunguko wa kwanza.

Wachezaji wa timu ya Young Africans.

Young Africans ipo nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 18 ushindi 13 na sare tano ikiwa ni moja ya timu ambazo hazijapoteza mchezo wowote sawa na Azam huku ikiweza kukusanya alama 44.

Wachezaji wa Mbeya City.

Mbeya City ipo nafasi ya 13 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 18, ikishinda michezo minne, sare tano na kufungwa michezo tisa huku ikiweza kukusanya alama 17.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *