NYASI ZA MIKOA MITATU ‘KUWAKA MOTO’ LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inarejea leo baada ya mapumziko ya takribani siku 10 ambapo mzunguko wa 22 utaanza leo katika mikoa ya Arusha, Mbeya na Dar es Salaam.

Mchezo wa kwanza utakuwa mkoani Arusha ambapo Fountain Gate itaikaribisha timu ya Pamba Jiji katika uwanja wa Sheikhe Amri Kaluta majira ya saa 8:00 mchana.

Fountain Gate inashika nafasi ya 13 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 19 ushindi mitano, sare nne na kupoteza michezo 10 huku ikikusanya jumla ya alama 19.

Pamba Jiji ipo nafasi ya saba ikiwa imeshinda michezo sita, sare nane na kufungwa michezo mitano ndani ya michezo 19 ambayo timu hiyo imecheza huku ikikusanya alama 26.

Mchezo wa pili utakuwa majira ya saa kumi na robo ambapo Mbeya City itaikaribisha timu ya Mashujaa katika uwanja wa Sokoine.

Mbeya City ipo nafasi ya 14 Kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imecheza michezo 19 kushinda michezo minne, sare tano na kufungwa michezo 10 huku ikiweka kibindoni alama 17.

Mashujaa ipo nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imecheza michezo 19 ushindi nne, sare tisa na kufungwa michezo sita huku ikikusanya alama 21.

Mchezo wa mwisho utakuwa majira ya saa kumi na mbili jioni ambapo timu ya JKT Tanzania itakuwa mwenyeji wa KMC katika uwanja wa KMC Complex.

JKT Tanzania ipo nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imecheza michezo 19, ushindi saba,sare nane na kupoteza michezo minne .

KMC ipo nafasi ya 16 ikiwa imecheza michezo 19 ushindi miwili, sare tatu na kufungwa michezo 14.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *