LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo minne muhimu itakayochezwa ikiwa ni muendelezo wa mzunguko wa 23 katika viwanja tofauti huku kila timu ikisaka alama muhimu kuelekea mwisho wa msimu.
Timu za juu zinapigania ubingwa huku zile za chini zikihangaika kujinasua kwenye hatari ya kushuka daraja na kucheza Ligi ya Championship ya NBC.
Mchezo wa kwanza utawakutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya KMC katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro Majira ya saa nane mchana ambapo Mtibwa Sugar wanaingia wakiwa nafasi ya 11 kwenye msimamo huku KMC wakiwa nafasi ya mwisho.
Katika mchezo mwingine Tanzania Prisons watawakaribisha Fountai Gate kwenye uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya majira ya saa nane mchana katika pambano litakalokuwa na ushindani mkubwa.
Tanzania Prisons wanashika nafasi ya 15 huku Fountain Gate wakiwa nafasi ya 10 na alama 25 wakisaka kuendelea kubaki kwenye nafasi za juu za msimamo ili kuepuka kushuka daraja.
Mashujaa watakuwa na kazi ngumu dhidi ya timu ya Simba inayosaka taji la Ligi Kuu ya NBC baada ya misimu minne huku Mashujaa ikiwa nafasi ya tisa kwenye msimamo ikipambana kujihakikishia nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu ujao.
Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma majira ya saa 10 :15 jioni na unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora wa timu zote mbili msimu huu.
Katika mchezo mwingine wa kusisimua Azam FC watachuana na Pamba Jiji Katika uwanja wa Azam complex jijini Dar es salaam majira ya saa 12:30 jioni.
Azam wanaingia wakiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo huku Pamba Jiji wakiwa nafasi ya saba, kila mmoja akihitaji ushindi ili kutimiza malengo yake msimu huu.
Simba bingwa