MZUNGUKO wa 29 wa Ligi ya NBC Championship unaendelea leo kwa michezo nane itakayochezwa majira ya saa kumi jioni.
Mchezo wa kwanza utakuwa uwanja wa Majimaji ambapo Songea United itakuwa mwenyeji wa timu ya Hausung huku Ken Gold ikichuana na B19 kwenye uwanja wa Chunya mkoani Mbeya.
Polisi Tanzania itaikaribisha timu ya Mbeya Kwanza katika uwanja wa Usharika mkoani Kilimanjaro mchezo utakaokuwa mbashara kwenye chaneli ya FIFA +, huku African Sports ikimenyana na Bigman kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Kagera Sugar itachuana na Gunners katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera huku Stand United ikicheza na Geita Gold katika uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga.
TMA na Barberian zitacheza katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha huku Transit Camp ikichuana na Mbuni kwenye uwanja wa TFF Kigamboni.