MBILI ZA MOTO LEO LIGI KUU YA NBC.

MZUNGUKO wa 26 wa Ligi Kuu ya NBC unatamatika leo kwa michezo miwili itakayochezwa mkoani Dar es Salaam na Mbeya.

Wachezaji wa Simba.

Simba iliyopo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC inayosaka nafasi ya kutwaa ubingwa itakuwa mwenyeji wa timu ya Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza inayoshika nafasi ya saba ambapo timu hiyo inatafuta kujiimarisha katika nafasi nzuri huku mchezo huo ukitarajiwa kupigwa kwenye uwanja wa KMC Complex majira ya saa kumi jioni.

Wachezaji wa Pamba Jiji

Sambamba na mchezo huo Tanzania Prisons iliyopo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikisaka kujinasua kushuka daraja itaikaribisha timu ya Dodoma Jiji inayoshika nafasi ya nane kwenye msimamo wa Ligi hiyo ambayo pia inatafuta kujiweka katika nafasi nzuri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *