LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2026/27 KUANZA LEO.

Pazia la Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027 linafunguliwa rasmi leo kwa michezo mitatu itakayochezwa katika viwanja mbalimbali nchini.

Mchezo wa kwanza utakuwa jijini Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba majira ya saa nane mchana ambapo timu ya Pamba Jiji itakuwa mwenyeji wa timu ya Dodoma Jiji huku mchezo huo ukitarajiwa kuwa na upinzani mkubwa kutokana na timu zote mbili kutaka alama hizo ili kuanza kujiweka katika nafasi nzuri.

Mchezo wa pili utakuwa jijini Mbeya katika uwanja wa Sokoine ambapo timu ya Mbeya City itakuwa mwenyeji wa timu ya Geita Gold iliyorejea Ligi Kuu baada ya kuwa mabingwa wa Ligi ya Championship msimu uliopita mchezo huo utakuwa majira ya saa kumi na robo jioni.

Mchezo wa mwisho utakuwa majira ya saa moja jioni ambapo timu ya Singida Black Stars itakuwa mwenyeji wa timu ya Fountain Gate katika uwanja wa Airtel mkoani Singida.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *