NAMUNGO, FOUNTAIN ZATAMBA NYUMBANI LIGI KUU YA NBC.

 

Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/27 imeendelea jana kwa mzunguko wa pili kwa kuzikutanisha timu za Fountain gate na Mashujaa mchezo wa mapema saa 10:00 alasiri mkoani Arusha,huku mchezo mwingine ukichezwa saa 1:00 usiku mkoani Lindi ukiwakutanisha Namungo na Geita Gold.

Katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Fountain Gate ilikusanya alama tatu muhimu kwa bao la Kassim Shaban dakika ya 10.

Bao hilo lilitosha kuipa Fountain Gate alama muhimu mbele ya mashabiki wake, huku Mashujaa ikishindwa kupata bao la kusawazisha hadi filimbi ya mwisho na kuondoka ugenini mikono mitupu.

Mchezo mwingine uliopigwa Uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi uliwakutanisha Namungo na Geita Gold, ambapo wenyeji Namungo walitumia vyema faida ya uwanja wa nyumbani na kupata ushindi wa bao 1-0.

Hashimu Manyanya ndiye aliyekuwa shujaa wa Namungo baada ya kuifungia timu yake bao la ushindi dakika ya 25, bao lililodumu hadi mwisho wa mchezo.

Geita Gold, licha ya jitihada za kutafuta bao la kusawazisha, haikuweza kupata matokeo na hivyo kulazimika kuondoka Lindi bila alama.

Matokeo hayo yamezifanya Fountain Gate na Namungo kuanza safari kwa ushindi wa nyumbani huku Mashujaa na Geita Gold zikipoteza alama ugenini.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *