CHAMPIONSHIP 2026/27 KUANZA RASMI LEO.

Ligi ya Championship ya NBC msimu 2026/27 inaanza rasmi leo kwa michezo mitatu itakayochezwa katika viwanja tofauti huku timu zikianza safari ya kuwania nafasi za kupanda Ligi Kuu ya NBC.

Mchezo kwanza utapigwa katika uwanja wa Ali hassan Mwinyi mkoani Tabora timu ya Rhino Rangers itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons kwenye mchezo utakaorushwa mubashara kupitia chaneli ya FIFA+.

Dar es salaam, KMC itawakaribisha Mbuni katika uwanja wa KMC katika mchezo utakaoonyeshwa kupitia Ligi Kuu TV kupitia mtandao wa youtube.

Katika mchezo mwingine katika mkoa wa Dar es salaam kigamboni united itakuwa mwenyeji wa TMA katika uwanja wa uhuru , na michezo yote itapigwa saa 10:00 alasiri.

Ufunguzi huo unatarajiwa kuleta ushindani mkubwa kutokana na kila timu kuanza msimu zikiwa na malengo mapya huku mashabiki wakisubiri kuona kiwango cha timu zao baada ya maandalizi ya msimu mpya.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *