LIGI Kuu ya NBC imeendelea kushika kasi ikiwa ni mzunguko wa sita wa ligi hiyo ambapo timu ya Yanga itaikaribisha timu ya Geita Gold katika uwanja wa KMC leo saa 1:00 usiku.
Mchezo huu unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili ambazo zimeanza vema msimu zikipambana kupata alama muhimu mwanzoni ili kujiweka katika nafasi nzuri.
Timu ya Yanga ndio inashika nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi huku Geita Gold ikishika nafasi ya sita hivyo timu hizo zinatarajiwa kucheza kwa ushindani mkubwa ili kutopoteza alama za mchezo na kuendelea kushika nafasi nzuri zaidi.
Ikimbukwe kuwa Yanga imecheza michezo mitano na kushinda yote huku Geita Gold ikishinda michezo miwili, kusare mmoja na kupoteza miwili katika michezo mitano aliyoicheza ya ligi kuu ya NBC 2026/2027.
Katika mchezo wa mwisho Yanga amepata ushindi wa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya Fountain Gate huku Geita Gold akipoteza kwa mabao mawili kwa sifuri katika mchezo wake na Simba.