HAPATOSHI KWA MKAPA LEO

Dar es Saalam na viunga vyake itasimama kwa dakika 90 kupisha mchezo wa kwanza wa ‘derby’ ndani ya msimu huu wa 2022/2023 ukizikutanisha Yanga SC na Azam FC katika uwanja wa Benjamin Mkapa leo Septemba 6, 2022 saa 1:00 usiku.

Mara ya mwisho  timu hizi zilikutana Aprili 6, 2022 katika uwanja wa Azam Complex Chamazi na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, mabao ya Yanga yalifungwa na Djuma Shabani na Fiston Mayele huku lile la Azam likifungwa na Rodgers Kola.

Ni wachezaji wanne tu kwa kila timu ambao walishiriki katika mchezo wa mwisho timu hizi zilipokutana lakini hivi sasa hawapo na timu hizo, kwa upande wa Yanga wachezaji hao ni Deus Kaseke, Saido Ntibanzokiza, Balama Mapinduzi na Yassin Mustafa huku kwa upande wa Azam wakiwa ni Mudathir Yahya, Charles Zulu, Mathias Kigonya na Never Tigere.

Azam ndio timu ya mwisho kuifunga Yanga kwenye Ligi Kuu kwa bao 1-0, bao lake Prince Dube walipofanya hivyo kwenye msimu wa 2020/2021, baada ya hapo Yanga wamecheza michezo 39 kwenye Ligi Kuu bila kupoteza.

Je ni Yanga kuendeleza rekodi ya kutokufungwa   ama Azam kutibua rekodi hiyo?.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *